Yemen yazidi kutwama- Baraza
Hali nchini Yemen inazidi kuwa mbaya na ya machungu huku raia wakilipa gharama ya mapigano yanayoendelea kwa miaka miwili sasa.
Rais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa mwezi huu wa Machi, Balozi Matthew Rycroft wa Uingereza amesema hayo akizungumza na waandishi wa habari hii leo baada ya kikao cha faragha cha baraza hilo kilichoangazia Yemen.