Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Mashambulizi dhidi ya Allepo ni uhalifu wa kivita: Ripoti

Mapigano ya kuudhibiti mji wa Aleppo nchini Syria mwaka jana, yamesababisha mateso makali yanayochochea uhalifu wa kivita wameonya leo wachunguzi wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa.

Ikitumia shuhuda 300 za picha za setilaiti na sauti nyingine, ripoti ya kamisheni ya uchunguzi imeonyesha jinsi gani ndege za kivita za Syria na Urusi zilivyogeuza Mashariki mwa Aleppo kuwa mahame huku vikosi vya upinzani vikidaiwa kuporomosha mabomu katika maeneo yenye idadi kubwa ya watu ambayo yanadhibitiwa na vikosi vya serikali.