Sasa tuna uwezo wa kutuma haraka kikosi imara- Ladsous
Mkutano wa viongozi uliofanyika miaka miwili iliyopita kuhusu ulinzi wa amani uliboresha operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa.
Hervé Ladsous, mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa amesema hayo akihojiwa na Idhaa ya umoja huo, wakati huu ambapo anamaliza muda wake hii leo tarehe 31 mwezi Machi.
Amesema mkutano huo ulipitisha hatua ambazo kwazo hivi sasa zimeimarisha ulinzi wa amani, mathalani..
(Sauti ya Ladsous)