Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Sasa tuna uwezo wa kutuma haraka kikosi imara- Ladsous

Mkutano wa viongozi uliofanyika miaka miwili iliyopita kuhusu ulinzi wa amani uliboresha operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa.

Hervé Ladsous, mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa amesema hayo akihojiwa na Idhaa ya umoja huo, wakati huu ambapo anamaliza muda wake hii leo tarehe 31 mwezi Machi.

Amesema mkutano huo ulipitisha hatua ambazo kwazo hivi sasa zimeimarisha ulinzi wa amani, mathalani..

 (Sauti ya Ladsous)

ITU yaunda kikosi cha kuboresha miji.

Shirika la Umoja wa Mataifa la teknolojia ya taarifa na mawasiliano ITU limeunda kikosi lengo kwa ajili ya kutafiti uchakatuaji wa taarifa na usimamizi katika muktadha wa miji erevu, ili kufikia kiwango cha ITU.

Taarifa ya ITU inasema kwamba kundi hilo li wazi katika ushirikiano na kundi lolote linalohitaji kufanya hivyo ili kufanikisha ujumuishwaji wa teknolojia ya taarifa na mawasiliano (ICTs) katika mifumo ya miji na kuweka ramani za miji duniani.

Syria ondoeni vikwazo vya kiutendaji ili misaada ifike- UM

Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo wamepokea taarifa kuhusu hali ya kibinadamu nchini Syria ambapo wameelezwa kuhusu vizuizi vinavyoendelea kukwamisha misafara iliyobeba misaada ya kibinadamu.

Rais wa Baraza hilo kwa mwezi huu wa Machi, Balozi Matthew Rycroft wa Uingereza ameeleza hayo akizungumza na waandishi wa habari baada ya kikao kilichohutubiwa na mkuu wa masuala ya usaidizi wa dharura kwenye Umoja wa Mataifa Stephen O’Brien. Balozi rycroft amesema..

(Sauti ya Balozi Rycroft)

Mgogoro wa wakimbizi wahitaji wajibu wa pamoja-Hendricks

Balozi mwema wa heshima ya maisha wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR Barbara Hendricks ametoa wito kwa Muungano wa Ulaya kukumbuka maadili ya kuanzishwa kwake.

Akizungumza kwenye bunge la Muungano wa Ulaya kwenye maadhimisho ya miaka 60 ya mkataba wa Roma ametoa wito kwa nchi wanachama kutimiza wajibu wao katika kushughulikia changamoto ya kimataifa ya wakimbizi.

Ahadi ya kupatia makazi wakimbizi wa Syria yasuasua- UNHCR

Wakati idadi ya watu wanaokimbia Syria ikivuka milioni 5 kutokana na vita vilivyodumu miaka sita, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limetaka jamii ya kimataifa ichukue hatua zaidi kuwasaidia wapate hifadhi.

Kaminshna Mkuu wa UNHCR Filippo Grandi amesema bado kuna safari ndefu kupanua wigo wa makazi kwa wakimbizi hao wanawake, wanaume na watoto.

Ziara yangu Iraq ni kuonyesha mshikamano:Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema yuko nchini Iraq kuonyesha mshikamano wake na watu na serikali ya taifa hilo lililoghubikwa na vita.

Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa pamoja na waziri mkuu wa Iraq Haider al-Abdi, amesema ana matumaini mji wa Mosul utakombolewa kabisa hivi karibuni na ameipongeza serikali kwa juhudi zake za kutaka

(Sauti ya Guterres CUT 1)

UNESCO yamtunuku mwandishi Dawit Isaak mzaliwa wa Eritrea

Dawit Isaak, mwandishi wa habari mzaliwa wa Eritrea mwenye uraia wa Sweden ambaye sasa yuko kifungoni, amechaguliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni UNESCO , kupokea tuzo ya kimataifa ya uhuru wa vyombo vya habari kwa mwaka 2017 ijulikanayo kama UNESCO/Guillermo Cano World Press Freedom Prize.

Bwana. Isaak alikamatwa katika msako wa vyombo vya habari uliofanyika Septemba 2001. Mara ya mwisho alisikika 2005, na wapi aliko sasa ni kitendawili kisicho na jibu.

Kubiš alaani vikali shambulio la kigaidi Yousufiyah Baghdad

Mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Iraq Ján Kubiš, amelaani vikali shambulio la kigaidi lililotokea Yousufiyah Baghdad nchini humo Jumatano jioni, ambapo watu kadhaa wameuawa au kujeruhiwa.

Bwana Kubiš amesema shambulio hilo la kinyama ni la pili kuilenga Baghdad chini ya siku kumi na limetekelezwa na magaidi wenye lengo la kulipiza kisasi kutokana na kushindwa kwenye mapambano mjini Mosoul na kwingineko.

David Beasley Mkurugenzi Mtendaji mpya wa WFP

Shirika la Mpango wa Chakula, WFP pamoja na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres wamemteua Bwana David Beasley wa Marekani kuwa mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo, akichukua nafasi ya Etherine Cousin ambaye anamaliza muhula wake wa miaka mitano Aprili 4 mwaka huu.

Taarifa ya WFP imesema Bwana Beasley ambaye ni Mwenyekiti wa kituo cha mikakati ya kimataifa na alichaguliwa kuwa mwakilishi wa baraza la wawakilishi wa la Marekani akiwa na umri wa miaka 21, ni mwenye uzoefu na sifa kubwa itakayonufaisha shirika hilo.

UNICEF yapongeza sheria ya Zampa nchini Italia

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesema sheria ya Zampa iliyopitishwa nchini Italia ni ya kihistoria katika ulinzi wa watoto wahamiaji na wakimbizi.

Watoto hao ni wale wanaokuwa wanasafiri wenyewe kuelekea Ulaya kusaka hifadhi ambapo UNICEF imesema ni ya kuigwa barani humo.

Mathalani sheria hiyo inataka kuwepo kwa msururu wa mikakati ikiwemo muda ambao watoto hao wanasubiri katika vituo vya mapokezi.

Halikadhalika inapigia chepuo huduma ya malezi na familia za wenyeji zinazoweza kuwachukua na kuwatunza.