Kila uwekezaji uwe jawabu kwa changamoto za mabadiliko ya tabianchi- Ban
Kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kumefanyika mkutano wa viongozi wa uwekezaji katika sekta binafsi lengo likiwa ni kuangalia hatari za mabadiliko ya tabianchi katika sekta ya biashara.
Akizungumza kwenye mkutano huo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema amesimama mbele ya wawekezaji hao akiwa na matumaini mapya kuwa ushirikiano kati ya sekta binafsi na umma unaweza kukabili changamoto ya mabadiliko ya tabianchi.