Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baada ya miaka Mitatu msaafara wa misaada wa UNHCR wawasili Deir Ez-Zor

Baada ya miaka Mitatu msaafara wa misaada wa UNHCR wawasili Deir Ez-Zor

Msafara wa kwanza wa misaada ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, umewasili  katika mji wa  Deir Ez-Zor uliopo  mashariki mwa Syria, baada ya miaka mitatau.

UNHCR inasema ,  malori matano ya misaada yaliwasili Deir Ez-Zor jana Septemba 14 baada ya safari ya saa 22 kutoka  kwenye ghala la UNHCR huko Homs. Msafara huo ulibeba vifaa muhimu vya kujikimu vya ujenzi, mahema, taa zitumiazo mwanga wa jua, vifaa vya  jikoni na usafi  vinavyokadiriwa kuwahudumia watu 30,000.

Halikadhalika kuna watu 93,000 huko Deir Ez-Zor  ambalo ni  jiji kubwa zaidi mashariki mwa Syria linalozingirwa  na waasi tangu  na  2014. Msaada wa awali umepelekwa kwa njia ya anga na  WFP , kabla ya  ngome  ya waasi kubomolewa na kuruhusu  mashirika ya misaada kuwafikia  anagalau watu 75000 amabo ni wahitaji wa misaada ya kibinaadamu huko Deir Ez-Zor.

Kutokana na hali ya kiusalama  kutoka miji ya Deir Ez-Zor na Ar-Raqqa UNHCR inasisitiza wito wake wa kulinda  walioko kwenye maeneo ya mgogoro na kuzitaka pande husika  kuheshimu  kanuni za kimataifa za kibinadamu. Zaidi ya raia wa Syria milioni 4.5 bado wapo kwenye maeneo yenye migogoro na yasiyofikika .