Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mbio zatumika Sudan Kusini kujenga maelewano baina ya jamii

Mbio zatumika Sudan Kusini kujenga maelewano baina ya jamii

Miaka sita ya uhuru wa Sudan Kusini ikitimu tarehe Tisa mwezi huu wa Julai, matumaini ya wananchi kuwa watakuwa na ustawi wa kudumu bado yako mashakani kutokana na mzozo unaoendelea nchini humo tangu mwezi disemba mwaka 2013.

Bado mamia ya watu ni wakimbizi wa ndani na wengine wanakimbilia nchi jirani, jamii mbali mbali zikiendelea kufarakana. Hata hivyo Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na wadau wake wameamua kutumia mbinu mbali mbali ili kuleta jamii pamoja na miongoni mwao mbinu hizo inasimuliwa na Selina Jerobon kupitia makala hii.