Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vijana Tanzania wachukua mwongozo kwa masuala mbali mbali ya dunia

Vijana Tanzania wachukua mwongozo kwa masuala mbali mbali ya dunia

Kongamano la kimataifa la vijana limeanza leo Jumatatu kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa .Mada kuu ya kongamano hilo linalowaleta pamoja viongozi vijana kutoka nchi mbalimbali, viongozi wa serikali, na asasi za kiraia ni jukumu la vijana katika kutokomeza umasikini, na kuchagiza maendeleo katika dunia inayobadilika.

Vijana wanapata fursa ya kujadili na kushauriana mada hizo sanjari na ujumuishaji wa maendeleo endelevu na changamoto kubwa zinazokabili vijana kama ajira.

Ahmad  Alhendawi ni mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu kuhusu vijana

(ALHENDAWI  CUT)

“Umuhi mu wa  kongamano hilo la ecosoc la vijana ni  kwamba  sasa linakwenda sanjari  na utekelezaji wa ajenda ya malengo ya maendeleo endelevu, fursa kwa viongozi  vijana na nchi wanachama  kuja  pamoja  na kujadili masuala ynayowahusu vijana  na  utekelezaji  wake.”

Naye kijana Peter Siniga ni kiongozi kijana kutoka Tanzania anasema

(SAUTI YA PETER SINIGA)