Harakati za kisomo nchini Tanzania
Kisomo! Yaani kujua kusoma na kuandika ni suala linaloelezwa kuwa ni kitovu cha mafanikio ya utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Katika siku ya kimataifa ya kisomo wiki hii, Umoja wa Mataifa umetaka hatua zichukuliwe kuimarisha kisomo kwa watu wazima, vijana na watoto. Hii ni kwa sababu miaka 50 tangu kuanza kuadhimishwa kwa siku hiyo, watu zaidi ya milioni 750 hivi sasa ulimwenguni kote hawajui kusoma na kuandika.Nchini Tanzania hatua zinachukuliwa na Nicholous Ngaiza wa radio washirika wa radio washirika Kasibante FM mkoani Kagera, anaangazia hali iko vipi mkoani humo.