Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali Darayya ni mbaya- de Mistura

Hali Darayya ni mbaya- de Mistura

Nchini Syria, hali halisi katika jimbo la Daraya ni hatari na ya kutisha amesema mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Syria, Staffan de Mistura. Taarifa zaidi na Amina Hassan.

 (Taarifa ya Amina)

Katika taarifa yake, de Mistura amesema  tangu mwezi Novemba  mwaka 2012  kumekuwepo na wito wa kuondoa kuzingirwa kwa eneo hilo, lakini halisikilizwi, halikadhalika wito wa kusitisha mapigano.

Mjumbe huyo ameongeza kuwa amejulishwa kuhusu makubaliano yaliyofikiwa usiku ya kuhamisha raia na wapiganji kuanzia leo jambo ambalo amesema Umoja wa mataifa haukuhusishwa na pande zote mbili.

Hata hivyo amesema ni muhimu sana kulinda wakazi wa  Darayya katika operesheni  hiyo na kwamba mchakato huo ufanyike kwa hiyari.

Bw.Bw. Staffan de Mistura anamsiihi mwenyekiti mwenza wa maswala ya kuleta amani Syria pamoja na  wajumbe wa patanishi kulitilia msisitizo swala la utekelezaji wa mkataba huu na matokeo katika viwango vya umoja wa mataifa.