Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNDP kukwamua wajasiriamali

UNDP kukwamua wajasiriamali

Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa, UNDP  kwa kushirikiana na washirika wa maendeleo umeanzisha mpango utakawawezesha wajasiriamali na sekta binafsi kwa ujumla kukuza kipato  kwa haraka na kwa njia rahisi.

Mpango huo unaofahamika kama wito wa hatua za kibiashara ni mahususi kwa ajili ya kupambana na umaskini na  unalenga zaidi kukuza vipato vya wajasiriamali wadogowadogo mathalani  biashara ya kutuma hela kwa kupitia  mitandao ya simu inayoshamiri kwa kasi barani Afrika.

Kwa mujibu wa Meneja wa mpango huo Sahba Sobhani jitihada hizo zitasaidia sekta binafsi katika kupambana na umaskini kwa kusaidia wajasiriamali kwa mifano njia sahihi za kupata masoko.

Miongoni mwa washirika wa kimaendeleo ktika mkakati huo ni Shirika la kimataifa la maendeleo laAustralia, Wizara ya mambo ya nje ya Uhollanzi  pamoja na Shirika la Maendeleo la marekani USAID.