Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tushirikiane kudhibiti usafirishaji haramu baharini: UNHCR

Tushirikiane kudhibiti usafirishaji haramu baharini: UNHCR

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa juu wa wakimbizi, Antonio Guterres,amerejelea wito wake akizitaka nchi zilizoko katika eneo la Asia Pacific kuanzisha mashirikiano ya pamoja ili kukabiliana na wimbi la watu wanaopoteza maisha wakati wakiwa kwenye misafara ya kimagendo katika bahari ya Hindi.  Ametoa wito huo wakati UNHCR ikiandaa mkutano utakaofanyika mwezi huu huko Indonesia kujadili jinsi ya kukabiliana na wimbi la misafara haramu katika eneo la Asia-Pacific. Taarifa zaidi na George Njogopa.

(SAUTI YA GEORGE)