Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Graziano ataka kujitolea kwa mataifa katika kuangamiza njaa duniani:FAO

Graziano ataka kujitolea kwa mataifa katika kuangamiza njaa duniani:FAO

Mkurugenzi mkuu wa shirika la kilimo na mazao la Umoja wa Mataifa FAO Jose Graziano da Silva amesema kuwa ikiwa mataifa yataweka jitihada zao katika kumaliza njaa lengo la maendeleo ya milenia la kupunguza kwa nusu idadi ya watu wenye njaa duniani ifikapo mwaka 2015 bado litatimizwa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano kuhusu usalama wa chakula duniani da Silva amesema kuwa hatua muhimu zimepigwa katika kupunguza idadi ya watu walio na njaa kwa watu milioni 132 tangu mwaka 1990. Ameongeza kuwa bado watu milioni 870 wanatatizwa na njaa wakati mikakati ya kupunguza njaa ikiwa imekwama tangu mwaka 2007. Jason nyakundi na taarifa kamili.

(SAUTI YA JASON NYAKUNDI)