Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uchaguzi wa madiwani waahirishwa Burundi hadi wiki ijayo

Uchaguzi wa madiwani waahirishwa Burundi hadi wiki ijayo

Nchini Burundi, uchaguzi wa madiwani ambao ungefanyika leo umeakhirishwa hadi jumatatu ijayo tarehe 24 Mai.

Tume huru ya uchaguzi nchini humo  imesema sababu ya kuahirisha uchaguzi  ni matatizo ya kiufundi hasa usumbufu  wa kuwasilisha upatikanaji  wa kadi za kupigia kura za vyama mbalimbali. Ni wananchi milioni tatu  na laki 6 wanaotarajiwa kushiriki mchakato mzima wa uchaguzi .

Uchaguzi wa madiwani utakuwa wa kwanza kwenye mlolongo wa chaguzi tano ukiwemo ule wa urais utakaofanyika tarehe 28 mwezi wa Juni mwaka huu. Kutoka Bujumbura,muandishi wetu Ramadhani Kibuga ametuandalia ripoti hii.