Maelfu na maelfu ya wakimbizi kupata mikopo
Maelfu na maelfu ya watu walopoteza makazi yao kote duniani watapata mikopo midogo ili kuweza kuanzisha biashara zao wenyewe na kuweza kujitegemea, kufuatia makubaliano kati ya Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji UNHCR na shirika la kutoa mikopo midogo iliyoanzishwa na mshindi wa tunzo ya Nobel Muhammad Yunus kutoka Bengladesh Grameen Trust.