Ukosefu wa ajira unaathiri jamii asilia hususani vijana
Vijana wa kimaasai huathirka sana kwa kukosa kazi na wanatumbukia katika majanga kama vile kuuza madawa ya kulevya, ni kauli ya mwakilishi wa jamai ya kimasaai kutoka Tanzania aliye pia mwakilishi wa shirika la maendeleo ya wanawakwe wamaasai MWEDO, Ndinini Kimesirasika.
Katika mahojiano na Joseph Msami wa idhaa hii kandoni mwa kongamano la 14 la watu wa asili linaloendelea mjni New York Bi Ndinini amesema pia jamii hizo zinakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwamo ukosefu wa elimu. Kwanza anaanza kueleza ujumbe wa MWEDO katika kongamano.