Muziki waleta nuru kwa wakimbizi wa Syria nchini Ugiriki
Pakua
Vita nchini Syria vimeingia mwaka wa 7 na mamia ya maelfu ya raia wamekimbia nchi hiyo kwani si shwari tena. Maisha ambayo wananchi walikuwa wamezoa yametumbukia nyongo. Hata hivyo hata kule walipo wanatafuta mbinu ya kuweza kuishi na kutumia stadi zao ili kukabiliana na machungu. Miongoni mwao ni mkimbizi kutoka Syria aliyeko Ugiriki ambaye anatumia ujuzi wake. Je anafanya nini? Ungana basi na Assumpta Massoi kwenye makala hii.