Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

DR Congo

Innoss B(kushoto) na Mkurugenzi wa WFP DRC, Peter Musoko(Kulia). Innoss B akitia saini barua rasmi ya kuteuliwa kama Msaidizi wa Ngazi ya Juu wa WFP nchini DRC, akihimiza milo yenye afya na lishe bora.
© WFP/Charly Kasereka

Innoss’B kutumia muziki kusongesha elimu na lishe bora DRC

Nimeshuhudia njaa mara nyingi sana wakati wa utoto wangu, kabla ya kwenda shule tulikuwa na njaa na kabla ya kulala tulikuwa na njaa, ndivyo asemavyo mwanamuziki Innocent Balume, al maaruf Innoss’B ambaye ametangazwa kuwa muungaji mkono wa ngazi ya juu wa shirika la  Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP katika kusongesha milo yenye afya na lishe bora nchini mwake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Sauti
2'6"
Kamanda wa TANZBATT-10, Luteni Kanali John Peter Kalabaka akimkabidhi bendera ya Tanzania Luteni Kanali  Vedasto Ernest Kikoti ikiwa ni ishara ya kukabidhiana majukumu ya ulinzi wa amani huko Beni Mavivi jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokra…
TANZBATT-10

Wananchi DRC eleweni na ikubalini dhamira ya UN ya kulinda raia - TANZBATT-11

Hii leo huko jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kikosi cha 10 cha Tanzania (TANZBATT-10)  kilichoko kwenye brigedi ya mapigano (FIB) ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO imekabidhi majukumu kwa kikosi cha 11, TANZBATT-11, katika hafla iliyofanyika eneo la Beni-Mavivi. Msimulizi wetu ni Kapteni Abubakari Muna, Afisa Habari wa TANZBATT-10.

Sauti
3'28"