Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

elimu

Coletha Magreth binti mkimbizi kutoka DRC ambaye anaishi katika makazi ya Wakimbizi Hoima nchini Uganda.
UN News

UN ikiadhimisha miaka 80 wakimbizi wasihi kupatikana kwa amani ya kudumu ili warejee makwao

Dunia ikiadhimisha siku ya Umoja wa Mataifa tarehe 24 Oktoba ambapo inatimiza miaka 80 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1945 huko San Fransisco nchini Marekani mara baada ya kumalizika kwa vita kuu vya pili vya Dunia ambapo mpaka sasa una jumla ya nchi wanachama 193, wananchi wameomba juhudi zaidi zifanyike ili kumaliza vita na wakimbizi waweze kurejea katika nchi zao.

UN News

UN Tanzania yatoa elimu ya amani na utangamano kwa wanafunzi kuelekea

Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Amani, hapo Jumapili tarehe 21 mwezi Septemba 2025, Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kwa kushirikiana na baadhi ya wadau nchini humo, umeendesha warsha ya siku moja ya kutoa elimu kwa wanafunzi wa shule ya msingi Hazina jijini Dar es Salaam kuhusu ya umuhimu wa kuishi kwa amani na kuchukua hatua sasa katika kuidumisha.

Sauti
2'30"
Wanafunzi wa darasa la 7 katika Shule ya Msingi ya Zanaki jijini Dar es Salaam, Tanzania.
World Bank/Sarah Farhat

UN Tanzania yatoa elimu kwa wanafunzi kuelekea maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Amani

Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Amani, hapo Jumapili tarehe 21 mwezi Septemba 2025, Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kwa kushirikiana na baadhi ya wadau nchini humo, umeendesha warsha ya siku moja ya kutoa elimu kwa wanafunzi wa shule ya msingi Hazina jijini Dar es Salaam kuhusu ya umuhimu wa kuishi kwa amani na kuchukua hatua sasa katika kuidumisha. Warsha hiyo imeongozwa na kauli mbiu  “Chukua hatua Sasa, kwa ajili ya Dunia yenye Amani.”

Sauti
2'30"
© UNICEF/Osman Khayyam

UNICEF yahimiza Taliban kuruhusu wasichana Afghanistan kuendelea na masomo

Tarehe kama ya leo, 18 Septemba mwaka 2021 dunia ilishitushwa na kuhuzunishwa na tangazo lililotolewa la uongozi wa Taliban nchini Afghanistan la kukataza wasichana barubaru kuendelea na masomo na kwamba darasa la sita ndio mwisho wa elimu yao. Sasa ni miaka minne na katazo hilo bado limesimama kitu ambacho Umoja wa Mataifa umeeleza kuwa ni “moja ya dhulma kubwa za wakati wetu.”  Leah Mushi na taarifa zaidi.

Sauti
2'42"
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa  wakishika doria sokoni nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR
© MINUSCA/Herve Serefio

MINUSCA na vikosi vya usalama vya ndani CAR waunganisha nguvu kuzuia ajali za barabarani

Kila mwaka,Wizara ya Uchukuzi na Usafirishaji wa Anga nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR,  kwa msaada wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MINUSCA,huandaa kampeni za usalama barabarani. Na hivi karibuni katika mji mkuu wa nchi hiyo,Bangui, MINUSCA kwa kushirikiana na Vikosi vya Usalama vya Ndani ISF wameungana kupambana na ajali za barabarani zinazoongezeka kila uchao,doria ya pamoja imefanyika kutoa elimu kwa watumiaji wa barabara.

Sauti
2'41"