Maambuki ya COVID-19 katika ukanda wa Afrika yameongezeka kwa kasi katika miezi miwili iliyopita, hali hiyo ikisisitiza hitaji la hatua za afya za umma zilizoimarishwa ili kuzuia kuongezeka kwa maambukizi, hasa wakati watu wanapokusanyika au kusafiri kwa sherehe za mwisho wa mwaka, imeeleza taarifa ya shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO, iliyotolewa hii leo mjini Brazzaville, Jamhuri ya Congo.