Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Usaidizi wa kibinadamu ni muhimu sana hasa kwa wakimbizi

Usaidizi wa kibinadamu ni muhimu sana hasa kwa wakimbizi

Pakua

Wahenga walinena siri ya mtungi aijuaye kata, hawakukosea kwani madhila ya mtu anayejua ni amsaidiaye. Na hili limethibitishwa na Bi Khadija Hussein, afisa wa masuala ya ulinzi wa wakimbizi kwenye kambi ya Dadaab nchini Kenya. Baada ya kuhudumu hapo kwa miaka mingi. Leo Bi khadija amemweleza Flora Nducha wa Idhaa hii kwamba sasa anatambua ni kwa nini kazi wanayoifanya kama wahudumu wa kibinadamu ina umuhimu mkubwa kwa maisha ya wakimbizi na kwa kwao pia na ndio maana siku ya kimataifa ya utu wa kibinadamu itakayoadhimishwa Agosti 19 ina maana kubwa..

Photo Credit
Wakimbizi kwenye kambi ya Dadaab nchini Kenya. Picha: UM/Video capture