Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN News

Ukiweza kutokomeza umasikini kwa wanawake, basi umeutokomeza kwa jamii: Paricia Makau

Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya wanawake, moja ya changamoto kubwa inayowakabili wanawake kote duniani ni umasikini na ndio maana Umoja wa Mataifa uliuweka kutokomeza umasikini kama lengo namba 1 la maendeleo endelevu SDGs. Na unashirikisha na kualika wadau mbalimbali kushirikia katika vita hiyo na wengi wameitikia wito likiwemo shirika la kimataifa la kujitolea lisilo la kiserikali lijulikanalo kama Voluntary service Overseas (VSO).

Sauti
4'53"
UN News/Anold Kayanda

Tunachotegemea baada ya LDC5 ni ushirikishwaji zaidi wa sisi vijana - Humphrey Mrema na Cosmas Msoma

Kwa mara ya kwanza katika historia ya miaka 50 ya mkutano wa nchi zenye maendeleo duni zaidi duniani, LDCs, vijana wamepewa kipaumbele cha juu baada ya mkutano huo kushirikisha vijana kutoka katika nchi mbalimbali ili wasaidie kuchangia mawazo ya namna bora ya kuondoa tatizo la uduni wa maendeleo duniani. Miongoni mwa vijana hao ni Cosmas Msoka na Humphrey Mrema ambao ni wawakilishi wa vijana wa Tanzania katika mkutano huo unaofanyika kila baada ya miaka 10 na sasa ukifanyika huko Doha, Qatar. Anold Kayanda wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa amezungumza nao.

Sauti
4'44"
UNDP/Sawiche Wamunza

Matunda ya ubia katika kuhifadhi wanyamapori wazaa matunda pori la Waga Tanzania

Nchini Tanzania kumulika ni kwa vipi mradi wa Jumuiya za Hifadhi za WAnyamapori, WMAs, unaotekelezwa kwa pamoja kati ya Wizara ya Maliasili na Utalii nchini humo na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo duniani, UNDP wa kuzuia ujangili na uhifadhi wa wanyamapori umesaidia jamii kunufaika sio tu na uwepo wa wanyamapori kwenye maeneo yao lakini pia kuishi kwa utangamano na wanyama kwa kuzingatia kuwa leo ni siku ya wanyamapori duniani na ujumbe ni ushirikishaji jamii katika hifadhi ya wanyamapori.

Sauti
5'35"
UNDP Guatemala/Caroline Trutmann

Baada ya hofu kubwa ya soko Peru, IFAD yaleta matumaini makubwa

Miaka miwili iliyopita, wakulima nchini Peru walikuwa na hofu ya kwamba janga la COVID-19 lingalifuta kabisa masoko yao waliyozoea kuuza mazao kama vile kakao na malimao. Walizoea kuuza sokoni lakini COVID-19 ilifuta masoko hayo kutokana na vizuizi vya kutembea.

Hata hivyo Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo, IFAD kupitia mradi wa kuchechemua kilimo vijijini baada ya COVID-19 ulileta nuru na sasa wakulima hawaamini kile wakipatacho. Ni kwa vipi basi? Ungana na Assumpta kwenye makala hii iliyoandaliwa na IFAD. 

Sauti
3'9"