Baada ya hofu kubwa ya soko Peru, IFAD yaleta matumaini makubwa
Pakua
Miaka miwili iliyopita, wakulima nchini Peru walikuwa na hofu ya kwamba janga la COVID-19 lingalifuta kabisa masoko yao waliyozoea kuuza mazao kama vile kakao na malimao. Walizoea kuuza sokoni lakini COVID-19 ilifuta masoko hayo kutokana na vizuizi vya kutembea.
Hata hivyo Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo, IFAD kupitia mradi wa kuchechemua kilimo vijijini baada ya COVID-19 ulileta nuru na sasa wakulima hawaamini kile wakipatacho. Ni kwa vipi basi? Ungana na Assumpta kwenye makala hii iliyoandaliwa na IFAD.
Audio Credit
Selina Jerobon/Assumpta Massoi
Sauti
3'9"