28 JUNI 2024
Pakua
- Bila uwekezaji mkubwa na kuongeza hatua, kufikiwa kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs kutasalia kuwa mgumu, imeonya Ripoti ya mwaka huu 2024 kuhusu mwenendo wa utekelezaji wa malengo hayo ikiwa imesalia miaka sita pekee kufikia muda ambao ulimwengu ulijiwekea kuwa umeyatimiza malengo yote 17.
- Huku takriban watu milioni 7 nchini Somalia wakihitaji msaada wa kuokoa maisha mwaka huu, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO linahimiza jumuiya ya kimataifa kuendelea kuunga mkono Wasomali wanaokabiliwa na athari za njaa,mabadiliko ya tabianchi, migogoro na kufurushwa makwao.
- Katika makala Assumpta Massoi kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Tanzania anamulika usaidizi wa shirika hilo kwa manusura wa mafuriko yaliyokumba taifa hilo la Afrika Mashariki.
- Mashinani tutasikia jinsi shirika la umoja wa mataifa la Afya ulimwenguni, WHO linakuza ubunifu miongoni mwa wanasayansi vijana wa afya barani Afrika ili kuboresha ufanisi, ubora wa huduma za afya na maendeleo katika matibabu na tiba.”
Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Audio Credit
Anold Kayanda
Audio Duration
9'59"