Wakimbizi 9,000 wameathirika na mafuriko makubwa yanayoendelea nchini Niger tangu mwezi Julai na sasa wengi wanahitaji msaada wa dharura sio tu wa huduma za chakula na afya bali pia malazi baada ya makazi yao kusambaratishwa kabisa na mafuriko hayo, limesema shirika la umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.