SHDEPHA+ yatekeleza kwa vitendo kauli ya UNAIDS ya jamii zishike hatamu kutokomeza Ukimwi
Leo ni siku ya Ukimwi duniani takwimu zikionesha kupungua sio tu kwa asilimia 70 ya vifo ikilinganishwa na mwaka 2004, idadi ilipokuwa kiwango cha juu zaidi duniani, bali pia maambukizi mapya ikilinganishwa na miaka ya 1980. Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la UNAIDS linasema miongoni mwa sababu za kupungua ni ushiriki wa jamii, yaani jamii kushika hatamu za vita dhidi ya Ukimwi.
24 NOVEMBA 2023
Hii leo jaridani tunaangazia amani na usalama katika ukanda wa Gaza na msaada wa kibinadamu nchini Chad. Makala tunakupeleka nchini Tanzania, na mashinani tunamulika Ibara ya 13 ya Tamko la Haki za Binadamu.
22 NOVEMBA 2023
Hii leo jaridani tunaangazia tunaangazia mizozo katika ukanda wa Gaza na hali ya mateka waliochukuliwa wakati wa shambulizi la Hamas huko Israel Kusini Oktoba 7. Pia tunamulika amani nchini Sudan Kusini. Makala tunakupeleka nchini Tanzania na mashinani Ufalme wa Tonga katika bahari ya Pasifiki, kulikoni?
Mataifa yaongeze kasi ya mabadiliko katika kuhakikisha upatikanaji wa choo safi na salama
Wakati hapo jana Novemba 19 dunia imeadhimisha Siku ya choo Duniani. maudhui yaliyobeba siku hiyo ni ‘Kuongeza kasi ya mabadiliko’. Kampeni hii inazingatia athari za janga la usafi wa mazingira ambalo huwa chanzo cha magonjwa mengi hasa ya kuambukiza. Kwa mujibu wa takwimu za shirika la afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO watu bilioni 3.6 karibu nusu ya watu wote duniani hawana huduma za msingi za usafi na milioni 494 miongoni mwao wanajisaidia haja kubwa katika maeneo ya wazi kwa kukosa huduma ya choo wengi wakiwa ni kutoka katika nchi masikini.
Juhudi za pamoja zimesaidia kudhibiti kipindupindu Zanzibar: WHO
Mtazamo wa kujumuisha sekta mbalimbali na kuishirikisha kikamilifu jamii imekuwa chachu kubwa ya kudhibiti milipuko ya ugonjwa wa kipindupindu iliyokuwa ikikiandama kisiwa cha Zanzibar kwa muda mrefu limesema shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO. Mtazamo huo ambao unaunganisha kampeni za uelimishaji kwa jamii kupitia ufadhili wa muungano wa chanjo duniani GAVI na msaada wa wadau mbalimbali likiwemo shirika la WHO imekisaidia kisiwa hicho kutokuwa na mgonjwa hata mmoja wa kipindupindu katika miaka mitano iliyopita. Ungana na Flora Nducha kwa makala hii kwa kina.