Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

António Guterres

Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, New York, USA.
UN Photo/Mark Garten

Guterres: Umoja wa Mataifa ni wenu tushirikiane

Leo umoja wa Mataifa unatimiza miaka 80 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1945 baada ya vita vikuu vya pili vya dunia. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametuma ujumbe wa siku hii akimihiza watu wote washirikiane katika kusongeza majukumu ya shirika hilo kwani ni lao.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amepongeza mazungumzo “yenye kujenga” kati ya viongozi wa Wacyprus Wagiriki na Wacyprus Waturuki baada ya mkutano wa ngazi ya juu uliofanyika leo Julai 17 katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini Ne…
UN Photo/Eskinder Debebe

Mgawanyiko wa Cyprus: Katibu Mkuu UN ahimiza majadiliano kuendelea kwa ajili ya amani

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amepongeza mazungumzo “yenye kujenga” kati ya viongozi wa Wacyprus Wagiriki na Wacyprus Waturuki baada ya mkutano wa ngazi ya juu uliofanyika leo Julai 17 katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani kwa lengo la kuendeleza juhudi za kuleta amani na kuaminiana katika kisiwa kilichogawanyika cha Cyprus.

Viongozi wa kimataifa wanaonesha mshikamano wao katika mkutano wa BRICS nchini Brazil.
United Nations/Ana Carolina Fernandes

Katibu Mkuu wa UN atoa wito kwa BRICS kuongoza kukabili mabadiliko ya tabianchi, afya na mageuzi ya ufadhili

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa wito mzito kwa viongozi wa dunia katika Mkutano  wa BRICS unaofanyika nchini Brazil, akihimiza kuchukuliwa kwa hatua za haraka na za pamoja katika kukabiliana na mizozo inayohusiana ya mabadiliko ya tabianchi, uharibifu wa mazingira, na afya ya umma.