Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hiI leo Machi 2 ametembelea eneo katika moja ya viwanja vya Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, ambalo limetumiwa na shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF, kutoa wito kuhusu dharura ya elimu iliyotokana na COVID-19 na kukuza ufahamu kuhusu uhitaji wa serikali kuzifungua shule.