Heko wanawake wa Somalia kwa mchango wa kulijenga vyema taifa lenu: UNSOM
Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya wanawake hii leo Mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia UNSOM, umewapongeza wanawake wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika kwa mchango wao mkubwa unaoendelea kwa ajili ya kusongesha maendeleo ya taifa hilo.