Chuja:

usawa wa kijinsia

15 Juni 2022

Jaridani Jumatano, Juni 15, 2022 na Leah Mushi

-Shida na changamoto nyingi zinazowakumba wanawake ni kutokana na mfumo dume na uchu wa madaraka: Guterres

-Mtoto asimulia safari ya Bunagana hadi Rutshuru nchini DRC

-Makala inamulika changamoto na jitihada za kufikia lengo la huduma za afya kwa wote nchini Tanzania kabla ya ukomo wa malengo ya maendeleo endelevu SDGs.

-mashinani tutaelekea katika Wilaya ya Kaabong, Mkoa wa Karamoja nchini Uganda kumsikiliza kijana aliyekuwa mchunga ng’ombe na sasa ameianza safari ya kuisaka elimu

Sauti
11'53"
United Nations

Unaelewa nini kuhusu “Usawa wa Kijinsia”? Baadhi ya vijana wanawake Tanzania wanaeleza

Umoja wa Mataifa unasema kuwa athari za kiuchumi na kijamii za janga la COVID-19 zimeathiri vibaya maendeleo ya hivi karibuni yaliyokuwa yamefikiwa katika usawa wa kijinsia. Unyanyasaji dhidi ya wanawake na wasichana umeongezeka, ndoa za utotoni zinatarajiwa kuongezeka baada ya kuwa zimepungua katika miaka iliyopita. Gonjwa hilo limeonesha hitaji la hatua za haraka kushughulikia kukosekana kwa usawa wa kijinsia ambao bado umeenea ulimwenguni kote na umuhimu wa kurejea kwenye mbio za kufikia usawa wa kijinsia.

Sauti
4'49"
Mlinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, katika kikosi cha tano, TANBATT-5 kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa unaolinda amani nchini Mali, MINUSCA, akimsaidia mwanamke kubeba maji.
Meja Asia Hussein/TANBATT-5

Tunaushukuru Umoja wa Mataifa na Jeshi la Tanzania kwa kuzingatia usawa wa kijinsia

Tukiwa bado tuko katika mwezi wa wanawake ambao umekuwa na matukio kadhaa makubwa kama maadhimisho ya siku ya kimataifa ya wanawake duniani na siku ya majaji wanawake, wanawake wanajeshi walinda amani kutoka Tanzania wanaohudumu katika kikosi cha 5 kutoka Tanzania kinacholinda amani kupitia mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, MINUSCAR, wameushukuru Umoja wa Mataifa pamoja na Jeshi lao la Tanzania kwa kuzingatia usawa wa kijinsia katika mipango ya ulinzi wa amani.

Sauti
3'6"