Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN kusaidia Tanzania kufanikisha Ajenda 2030

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres (kushoto) na Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania baada ya mazungumzo jijini New York, Marekani.
UN / Evan Schneider
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres (kushoto) na Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania baada ya mazungumzo jijini New York, Marekani.

UN kusaidia Tanzania kufanikisha Ajenda 2030

Malengo ya Maendeleo Endelevu

Mara baada ya kuhutubia mjadala mkuu wa mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA76 jijini New York, Marekani, Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania alikuwa na mazungumzo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.
 

Taarifa ya msemaji wa Umoja wa Mataifa iliyotolewa Alhamisi jijini New York, Marekani imesema katika mkutano huo, Katibu Mkuu Guterres amekaribisha marekebisho makubwa ya kisera yaliyofanyika hivi karibuni katika taifa hilo la Afrika Mashariki.

Marekabisho hayo ni pamoja na usimamizi na udhibiti wa janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19.

Halikadhalika walijadili suala la amani na usalama na changamoto zake katika ukanda wa Maziwa Makuu.

Katibu Mkuu Guterres amemhakikishia Rais Samia juu ya usaidizi wa Umoja wa Mataifa kwa Tanzania katika harakati zake za kufanikisha Ajenda 2030 ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.