Rais wa Baraza Kuu la UN, aitumia CHOGM kupeleka ujumbe mzito
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Abdulla Shahid yuko katika mji Mkuu wa Rwanda Kigali ambako unafanyika Mkutano wa 26 wa wakuu wan chi za Jumuiya ya Madola.
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Abdulla Shahid yuko katika mji Mkuu wa Rwanda Kigali ambako unafanyika Mkutano wa 26 wa wakuu wan chi za Jumuiya ya Madola.
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Abdulla Shahid akizungumzia hali inayoendelea Ukraine, ametoa wito wa kusitishwa mapigano mara moja na kurejea katika diplomasia na mazungumzo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaja mambo makuu matano anayoona yanapaswa kupatiwa kipaumbele ili dunia iweze kuwa na mwelekeo sahihi na mustakabali bora kwa kila mkazi wake.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio ambalo linalaani ukataaji na upindishaji wa suala la mauaji ya halaiki au holocaust.
Huku janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 likiendelea kusambaa maeneo mbalimbali duniani, Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Abdulla Shahid leo wakati akitoa hotuba ya vipaumbele vyake, amesisitiza umuhimu wa mshikamano na matumaini.
Rais Samia Suluhu Hassan akifafanua kuhusu usawa wa kijinsia katika uongozi na akianza kwa kujibu swali anavyoiangalia nafasi ya juu aliyonayo hivi sasa akiwa Rais wa Tanzania, anasema kazi hiyo si rahisi bila kujali jinsia.
Hatimaye mjadala mkuu wa mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA76 umefunga pazia leo Jumatatu katika makao makuu ya Umoja huo jijini New York, Marekani huku Rais wa Baraza hilo Abdullah Shahid akisema mkutano huo umefanyika kwa mafaniko makubwa katikati ya janga la Corona au COVID-19 huku akitaja sababu za mafanikio hayo kuwa ni hatua bora za kupunguza maambukizi na viwango vya juu vya chanjo.
Wakati wa hotuba yake kwenye mjadala mkuu wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hii leo Jumamosi , waziri mkuu wa serikali ya Haiti, Ariel Henry, ametaka suluhisho la kudumu lipatikane kwa changamoto ya uhamiaj, akitoa wito kwa jamii ya kimataifa kuboresha haraka hali ya maisha katika nchi zinazotoa wakimbizi wa kisiasa au kiuchumi.
Waziri mkuu wa India Narendra Modi ameliambia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hii leo katika mjadala mkuu wa wazi wa UNGA76 kuwa wakati India inafanya mageuzi, ulimwengu hubadilika.
Rais wa Taifa la Palestina Mahmoud Abbas ametoa wito kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kuitisha mkutano wa kimataifa kuhusu amani na ili kuhakikisha kuwa mpango huo hauna mkwamo Israel lazima iondoke kutoka Ukingo wa Magharibi wa mto Jordan, Ukanda wa Gaza na Yerusalem Mashariki katika kipindi cha mwaka mmoja.