Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Samia Suluhu Hassan

07 JULAI 2022

Hayawi hayawi sasa yamekuwa na leo jarida linajikita katika maadhimisho ya siku ya kiswahili duniani kuanzia habari kwa ufupi ambayo imebisha hodi Paris Ufaransa kwenye makao makuu ya shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, halikadhalika Zanzibar ambako huko Jumuiya ya Afrika MAshariki imekuwa na maadhimisho maalum bila kusahau kauli ya Gertrude Mongela kuhusu hatua ya Kiswahili kutambulika kimataifa.

Audio Duration
10'44"
Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania akihutubia mjadala wa viongozi kuhusu mshikamano kwenye mkutano wa COP26 huko Glasgow, Scotland
UN WebTV Video

Tunapimwa kwa vitendo vyetu na si kwa ahadi kubwa kubwa- Rais Samia

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amezungumza katika mjadala wa wazi wa viongozi kwenye mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, CO26 huko Glasgow, Scotland na kusema mshikamano na juhudi zao kama viongozi katika kukabili mabadiliko ya tabianchi vitapimwa si kwa ahadi kubwa wanazotoa kwenye mkutano huo bali kwa jinsi wanatekeleza vipengele vyote vya mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi.