Kutoka kupanga safari za ndege hadi kusambaza vifurushi vya mlo; UNWTO yachukua hatua
Kutoka kupanga safari za ndege hadi kusambaza vifurushi vya mlo; UNWTO yachukua hatua
Mapendekezo hayo ni sehemu ya kwanza ya matokeo ya vikao ya kamati ya kimataifa ya utalii iliyoundwa kushughulkia janga la sasa, ikijumuisha wawakilishi kutoka sekta ya utalii duniani pamoja na Umoja wa Mataifa.
Taarifa ya UNWTO iliyochapishwa katika wavuti wake inasema kuwa “Kwa kutambua kuwa sekta ya utalii ni moja ya sekta zilizoathiriwa zaidi duniani kutokana na janga la Corona, mapendekezo yanalenga kusaidia serikali , sekta ya binasi na jamii ya kimataifa kukabiliana na dharura isiyo ya kawaida ya kijamii na kiuchumi ambayo ni COVID-19.”
Mapendekezo hayo yako 23 lakini yamegawanywa katika sehemu kuu 3 ambazo ni;
1. Kushughulikia janga huku athari zikipunguzwa
Mapendekezo muhimu yanataka watu waendelee kutunza ajira zao, kusaidia waliojiajiri, kuhakikisha kuna fedha au ukwasi, kupitia upya kodi, husiana na kutunza kazi, kusaidia wafanyikazi waliojiajiri, kuhakikisha ukwasi, kukuza ustadi wa ujuzi na kufanya mapitio ya kodi, gharama na kanuni zinazohusiana na utalii. Mapendekezo haya yamezingatia hali ya sasa ya mdororo wa kiuchumi.
2. Kutenga mafungu ya fedha ili kuchochea ukwamukaji
Seti hii ya Mapendekezo inasisitiza umuhimu wa kutoa kichocheo cha kifedha, pamoja na sera nzuri za ushuru, kuondoa vizuizi vya kusafiri mara tu dharura ya kiafya inaporuhusu, kukuza uhamasishaji wa visa, kukuza uuzaji na ujasiri wa watumiaji, ili kuharakisha kuimarika. Mapendekezo hayo pia yanataka utalii uwekwe katikati ya sera za kitaifa za kuimarisha na mipango.
Ukurasa kuhusu virusivyacorona & taarifa mpya
Wasomaji wanaweza kupata taarifa na muongozo kuhusu mlipuko wa virusi vya corona (2019-nCoV) kutoka Umoja wa Mataifa, Shirika la afya duniani na mashirika mengine ya UN hapa. Kwa habari mpya kila siku kutoka UN News, bofya hapa.3. Kujiandaa kwa ajili ya kesho
Kusisitiza uwezo wa kipekee wa utalii wa kuongoza ukuaji wa ndani na kitaifa na kimataifa ambapo mapendekezo yanataka msisitizo mkubwa kuwekwa kwenye mchango wa sekta hiyo kwenye ajenda 2030 au malengo ya maendeleo endelevu, SDGs na kujenga mnepo kutokana na mafunzo yaliyopatikana na janga la sasa. Mapendekezo hayo yanataka serikali na watendaji wa sekta binafsi kuwa mipango ya utayari, na kutumia fursa hii kugeukia uchumi wa mzunguko.
Akizungumzia mapendekezo hayo, Katibu Mkuu wa UNWTO, Zurab Pololikashvili amesema , “mapendekezo haya mahususi yanapatia nchi orodha ya hatua zinazoweza kuchukuliwa kusaidia sekta yetu kuendeleza kazi na kusaidia kampuni zilizo hatarini kwa wakati huu. Kuzuia athari za ajira na ukwasi, kulinda walio hatarini zaidi na kujiandaa kukwamuka tena, mambo haya yote lazima yawe vipaumbele vyetu muhimu.”
Hata hivyo nyaraka yenye mapendekeo hayo itakuwa ikifanyiwa marekebisho kila wakati kuligana na mwelekeo wa janga la Corona na ukweli na uhalisia katika kila nchi.