Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kuwait yapokea fidia nyingine ya dola milioni 270-UN

Bendera ya Kuwait
UN News/Jing Zhang
Bendera ya Kuwait

Kuwait yapokea fidia nyingine ya dola milioni 270-UN

Masuala ya UM

Tume ya fidia ya Umoja wa Mataifa leo imelipa dola zingine milioni 270 kwa serikali ya Kuwait kama sehemu ya fedha za dai la fidia lililobaki la nchi hiyo.

Tume hiyo ya fidia ya Umoja wa Mataifa ilianzishwa mwaka 1991 baada ya vita kati ya Iraq na Kuwait kwa kufuata maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa namba 687 na 692 yote ya mwaka 1991 ili kushughulikia madai na kulipa fidia kwa ajili ya hasara na uharibifu uliotokea kwa watu binafsi, mashirika, serikali na mashirika ya kimataifa.

Na hii ilikuwa ni matokeo ya moja kwa moja ya uvamizi wa serikali ya Iraq na ukaliaji wa Kuwait uliofanyika kati ya a Agosti 1990 hadi 2 Machi 1991.

Tume hiyo ilipokea takribani madai milioni 2.7 na ilikamilisha tathimini ya madai yote mwaka 2005.

Karibu dola bilioni 52.4 zimelipwa kwa zaidi ya mashirika ya kimataifa na serikali 100 ambazo zimegawanywa kwa madai yapatayo milioni 1.5

Uvamizi wa Iraq Kuwait mbali ya kukatili maisha ya watu wengi ulisababisha uharibifu mkubwa wa nyumba, barabara, mitambo na miundombinu mingine muhimu.