Mabomu yanayolipuka na kusambaza vilipuzi vingine yameua na kujeruhi mamia ya raia nchini Ukraine tangu mwaka 2022: UNIDIR
Mabomu yanayolipuka na kusambaza vilipuzi vingine yameua na kujeruhi zaidi ya raia 1,200 nchini Ukraine tangu kuanza kwa uvamizi mkubwa wa Urusi mwezi Februari 2022, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na muungano wa mashirika yasiyo ya kiserikali unaoungwa mkono na Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Utafiti wa Udhibiti wa Silaha UNIDIR.