Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

iraq

Mabomu yanayolipuka na kusambaza vilipuzi vingine yanawezakuwa yalitumika Ukraine.
© UNOCHA/Adedeji Ademigbuji

Mabomu yanayolipuka na kusambaza vilipuzi vingine  yameua na kujeruhi mamia ya raia nchini Ukraine tangu mwaka 2022: UNIDIR

Mabomu yanayolipuka na kusambaza vilipuzi vingine  yameua na kujeruhi zaidi ya raia 1,200 nchini Ukraine tangu kuanza kwa uvamizi mkubwa wa Urusi mwezi Februari 2022, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na muungano wa mashirika yasiyo ya kiserikali unaoungwa mkono na Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Utafiti wa Udhibiti wa Silaha UNIDIR.

Watoto wakicheza mbele ya kituo cha polisi huko Gao ambacho kilishambuliwa na magaidi.
UN Photo/Marco Dormino

Afrika imekuwa kitovu cha ugaidi duniani: Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 10 wa Umoja wa Mataifa wa kamati Kamati ya Kuratibu Mkataba wa Kimataifa wa Kupambana na Ugaidi barani Afrika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, jijini New York, Marekani, amesema, "taharuki hii inayoongezeka inateketeza mamilioni ya Waafrika. Hii inajumuisha wanawake na wasichana, ambao wako katika hatari kubwa ya unyanyasaji wa kijinsia na kikatili. Katika bara zima, Da'esh, Al-Qaida na washirika wao wanatumia mienendo ya migogoro ya ndani na udhaifu ili kuendeleza ajenda zao, huku wakisambaratisha mfumo wa kijamii wa nchi nzima na machafuko, kutoaminiana na hofu.”