Guterres: Kuwaacha watu katika kambi ya Al-Hol kutajenga chuki kwa vizazi vijavyo
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameipongeza Iraq kwa kuwarejesha nyumbani raia wake kutoka kambi ya Al- Hol iliyoko kaskazini mashariki mwa Syria iliyokuwa ikiwashikilia watu wanaoshukiwa kuwa na uhusiano na wanamgambo wa kikundi cha ISIL, na kuzitaka serikali zingine "kuwajibika na kuchukua hatua".