Kuwait yapokea fidia nyingine ya dola milioni 270-UN
Tume ya fidia ya Umoja wa Mataifa leo imelipa dola zingine milioni 270 kwa serikali ya Kuwait kama sehemu ya fedha za dai la fidia lililobaki la nchi hiyo.
Tume ya fidia ya Umoja wa Mataifa leo imelipa dola zingine milioni 270 kwa serikali ya Kuwait kama sehemu ya fedha za dai la fidia lililobaki la nchi hiyo.
Mkutano wa 72 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umetamatishwa hii leo ambapo aliyekuwa rais wake Miroslav Lajčák ametaja mambo sita muhimu aliyobaini wakati wa uongozi wake tangu mwezi Septemba mwaka jana.
Katika Neno la Wiki hii leo tunaangazia neno “Yamini” na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania. Bwana Sigalla anasema neno "Yamini" lina maana zaidi ya moja, Mosi, yamini ni kiapo, pili, yamini ni mkono wa mtu wa upande wa kulia au mkono wa kuume na yamini pia ni ahadi aitoayo mtu ya kutenda haki au kuficha siri baada ya kupewa wadhifa fulani..
Msimu wa mvua na pepo kali unaokaribia pamoja na ghasia kwa upande mwingine ni mwiba kwa watoto zaidi ya 700,000 waliokumbwa katika mgogoro wa wakimbizi wa Rohingya.
Ukitaka kupanga miji vizuri, husisha wanawake! Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na makazi, UN-Habitat, Maimunah Mohd Sharif wakati akifungua mkutano wa tisa wa jukwaa la miji,WUF9 ulioanza leo huko Kuala Lumpur Malaysia.
Amesema ni muhimu kushirikisha wanawake katika upangaji miji ili kufanikisha lengo namba 11 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs kuhusu miji jumuishi akigusia nukuu aliyowahi kuelezwa kuwa..
(Sauti ya Maimunah Mohd Sharif)
Wana mradi wa kuruwitu kutoka Kilifi Mombasa nchini Kenya, wametoa wito wa kuhifadhi mazingira leo ili kuepuka athari zake katika kizazi kijacho. Shida Magunda na Katana Ngala Hinzano wako katika mradi wa kuhifadhi mazingira ya bahari Mombasa kwa kutumia uzalishaji wa samaki. Mradi wao ambao ni wa kwanza nchini Kenya pi umetunukiwa tuzo ya mazingira ya Equator inayotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP na Equator initiative. Wamezungumza na Flora Nducha na Katana Ngala anaanza kueleza historia ya mradi
Hali ya Burundi imetengamaa na ni wakati muafaka kwa raia waliokimbilia nchi jirani na nchi za nje kurejea nyumbani. Wito huo umetolewa leo na waziri wa mambo ya nje wa Burundi Alain Aimé Nyamitwe akihutubia mjadala wa wazi wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa New York Marekani.
Nyamitwe amesema pamoja na changamoto zingine za kiuchumi kama yalivyo mataifa mengine ya Afrika , nchi hiyo imejitahidi kusuhulisha hali ya mvutano wa kisiasa uliojitokeza mwaka 2015 na kusabababisha watu wengi kukimbia nchini humo.