Kuwait yaunga mkono juhudi za kupunguza njaa nchini Syria
Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa, FAO, hii leo mjini Cairo Misri na Roma Italia limekaribisha na kushukuru mchango wa dola milioni tatu kutoka Kuwait ili kuwasaidia watu 20,000 walioko katika hali ya hatari pamoja na ndugu zao nchini Syria.