Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kuwait

FAO yapokea msaadawa dola milioni 5 za kuisaidia Yemeni

Vita vimechangia kwa kiasi kikubwa kutokuwepo na uhakika wa chakula nchini Yemen, kwani wakulima kama raia wengine wamefungasha virago kukimbia machafuko. Sasa mashirika ya Umoja wa Mataifa kama la chakula na kilimo FAO yanafanya juu chini kuwasaidia wakulima kufufua kilimo  na misaada kutoa kwa wahisani inahitajika. Leo Kuwaiti imetoa dola milioni 5 zitakazopiga jeki nia ya FAO yemen.

Huko Kuwait, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres
UN/Stéphane Dujarric

UN yazindua mradi wa kukwamua ujenzi wa Iraq

Mkutano wa kujadili ujenzi mpya wa Iraq ukifanyika nchini Kuwait, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema licha ya uharibifu mkubwa uliosababishwa na vita nchini humo, bado wairaq wamejitahidi kutoa asilimia 80 ya misaada ya kibiandamu kwa ajili ya wenzao.