Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baada ya kusuasua WHO na wadau wazindua kampeni mpya  ya kutokomeza Malaria.

Mwanamke akifunga chandarua cha mbu baada ya kukipokea wakati wa kampeni ya kitaifa ya ugawaji vyandarua vya mbu kwenye kijiji cha Giema Dama Wilaya ya Kenema nchini Sierra Leone , June 2017
Picha na UNICEF/UNO72220/Phelps
Mwanamke akifunga chandarua cha mbu baada ya kukipokea wakati wa kampeni ya kitaifa ya ugawaji vyandarua vya mbu kwenye kijiji cha Giema Dama Wilaya ya Kenema nchini Sierra Leone , June 2017

Baada ya kusuasua WHO na wadau wazindua kampeni mpya  ya kutokomeza Malaria.

Afya

Kasi ya kupunguza visa vya malaria imesimama baada ya miaka mingi ya kupungua kwa visa hivyo kote duniani, kwa mujibu wa ripoti mpya ya malaria duniani 2018  iliyotolewa leo. 

Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyotolewa na shirika la afya ulimwenguni, WHO  wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya ya kupambana na  Malaria itakayosaidia kurejesha kasi ya kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo, vifo vitokanavyo na malaria na kasi ya mapambano katika mstari unaostahili    jitihada kubwa zinapaswa kufanyika katika uzuiaji n atiba, lakini pia uwekezaji  ili kuwalinda watu walio katika hatari ya kupata maradhi hayo.

Ripoti imetaja sababu za kupungua kwa kasi ya kudhibiti visa vipya vya malaria kuwa ni  pamoja na watu wengi barani Afrika kutotumia vyandarua vyenye viuatilifu wanapolala, nyumba kunyunyuziwa dawa za kuua mbu kama ilivyokuwa awali na wajawazito kutopatiwa  kwa kiasi cha kutosha huduma za kujinga na malaria. 

Dkt Kesete Admasu Mwandamizi Mkuu wa  ushirika wa RBM-Role back Malaria.akieleza kuhusu mkakati huo uliopewa jina “mzigo mkubwa na kishindo kikubwa” amesema unajikitakatika masuala manne muhimu.Kampeni hii ina misingi muhimu minne:kuamsha uhamasishaji wa kitaifa na kimataifa ili kupunguza vifo vitokanavyo na malaria; kuweka msukumo  kupitia matumizi ya kimkakati ya taarifa; kuweka mwongozo, sera na mikakati ambayo inaendana na mataifa yote yanayosumbuliwa na malaria  na pia utekelezaji wa mwitikio wa kitaifa ulioratibiwa.Lakini la msingi zaidi ni“Nguzo ya kwanmza ni utashi wa kisiasa, ili kuwezekza katika malaria,. Na pia kuhakikisha kuwa kuna azma mpya  ya uongozi wa kitaifa katika mataifa yanayohusika. Bila utashi wa kisiasa  itakuwa vigmu kufanikisha malengo yetu ya pamoja.”

Lengo kuu la mkakati huu amesema ni kupunguza vifo vya malaria kwa takriban asilimia 40 ifikapo mwaka wa 2020. Kwa mwaka wa pili mfululizo ripoti ya WHO imeonyesha kuwa idadi ya wanaoathirika  na malariainaongezeka. Mfano mwaka 2017 ilikadiriwa kuwepo  visa vya malaria  milioni 219 ilikilinganishwa na visa milioni 217 mwaka 2016. 

Mwaka 2017 kulikuwa na takriban asilimia 70 ya visa  malaria sawa na watu milioni 151 na vifo 274,000 vilitokea katika mataifa 10 ya Afrika na Asia. Barani Afrika mataifa hayo ni pamoja na Uganda na Tanzania , Msumbiji,  Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo DRC, -Niger, Nigeria, Ghana, Mali, Burkina Faso, na Cameroon.