Licha ya mafanikio sasa kuna hofu kuhusu Malaria- Ripoti
Idadi ya wagonjwa wa Malaria kwa mwaka 2016 iliongezeka kwa zaidi ya visa milioni 5 ikilinganishwa na mwaka 2015 na hivyo kutiwa hofu juu ya mafanikio yaliyopatikana katika kutokomeza ugonjwa huo.
Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya shirika la afya ulimwenguni, WHO iliyotolewa Jumanne ikiongeza kuwa hata idadi ya vifo vitokanavyo na Malaria vimesalia 445,000 ikiwa ni sawa na mwaka 2015.
WHO inasema kwa hali ilivyo sasa, dunia iko njiapanda na ni lazima hatua ichukuliwe ili kuepusha kurejea katika hali ya zamani na hivyo kushindwa kufikia lengo la kutokomeza Malaria ifikapo mwaka 2030.
Akizungumzia kutokupungua kwa visa vya Malaria, Dkt. Winnie Mpanju Shumbusho, ambaye ni mwenyekiti wa ubia wa kutokomeza Malaria duniani, RBM ameieleza idhaa hii kuwa.
(Sauti ya Dkt. Winnie Mpanju Shumbusho)
Na hivyo Dkt. Winnie anapendekeza ufadhili wa kifedha lakini ..
(Sauti ya Dkt. Winnie Mpanju Shumbusho)