Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Malaria

Akina mama waleta watoto wao kwa uchunguzi wa lishe katika kliniki tembezi ya afya katika jimbo la Kassala, Sudan.
© UNICEF/Osman

Mamilioni hatarini kutokana na milipuko ya magonjwa Sudan: WHO

Sudan, nchi iliyoghubikwa na vita, hivi sasa inakabiliwa na janga lingine la afya ambapo magonjwa ya kipindupindu, surua, homa ya kidingapopo na malaria vinazunguka katika majimbo kadhaa na mchanganyiko wa magonjwa haya yote na utapiamlo vinaweza kuwa na athari mbaya sana kwa mamilioni ya watu limeonya leo shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO.

Mtoto mwenye umri wa miezi sita akipimwa malaria baada ya kimbunga Freddy kusababisha mafuriko na uharibifu nchini Malawi.
© UNICEF/Thoko Chikondi

Chanjo mpya kwa ajili ya kuzuia malaria kwa watoto yaidhinishwa

Mapendekezo ya kuanza kutumia kwa chanjo mpya R21/Matrix-M yanafuatia ushauri kutoka kwa Jopo la ushauri wa kimkakati kwa Shirika la Afya Duniani WHO kuhusu masuala ya chanjo, SAGE na Kikundi cha Ushauri wa Sera ya Malaria (MPAG) na kuidhinishwa na Mkurugenzi Mkuu wa WHO kufuatia mkutano wake wa kawaida wa kila mwaka uliofanyika tarehe 25-29 Septemba.

Phiona anafanya kazi katika kituo cha afya nchini Uganda kama mwanaharaki wa rika ya akina mama, anasaidia kutoa mafunzo na kusaidia akina mama kujifungua watoto wasio na VVU.
© UNICEF/Karin Schermbrucker

Viongozi wa dunia na wadau washikamana kutaka fursa sawa ya huduma za afya kwa wote: UNITAID

Wakati wa mkutano mkuu wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa wa mwaka huu, viongozi wa dunia, wadau wa afya na wawakilishi wa jamii wanaungana na shirika la kufanikisha upatikanaji wa dawa na tiba kwa gharama nafuu UNITAID, kutoa wito wa upatikanaji wa haraka na usawa zaidi wa bidhaa za afya zinazookoa maisha ili kuendeleza mchakato wa kupambana na changamoto kubwa zaidi za leo za afya, ikiwa ni pamoja na afya ya uzazi ya mama na mtoto, kuzuia majanga, kujiandaa na hatyua za kukabiliana na majanga, na virusi vya ukimwi VVU, kifua kikuu na malaria.

22 AGOSTI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Mapigano yanayoendelea huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC yakiendeshwa na vikundi vilivyojihami vya waasi yanaendelea kufurusha watu kutoka makwao, na hivyo wakimbizi hao wa ndani kushindwa kujikimu maisha yao ya kila siku. Malazi ni shida, makazi ni shida, halikadhalika chakula. Maisha yanakuwa ni changamoto kila uchao. Hali hiyo iko dhahiri kabisa jimboni Kivu Kaskazini ambako hata hivyo hatua za shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani, WFP kwa wakimbizi Oicha zimeleta ahueni.

Sauti
9'59"
Mwanamke akipokea dawa ya kuzuia malaria katika kituo cha afya nchini Uganda
© UNICEF/Maria Wamala

Nchi 12 Barani Afrika kuanza kutoa chanjo ya Malaria

Nchi 12 katika barani Afrika zinatazamiwa kupokea dozi milioni 18 za chanjo ya kwanza ya malaria katika kipindi cha miaka miwili ijayo imeeleza leo taarifa ya pamoja iliyotolewa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Afya ulimwenguni WHO na linaloshughulika na watoto UNICEF huku wakishirikiana na Ubia wa chanjo duniani, GAVI. 

Mjumbe wa timu ya afya ya kijiji VHT, Fenehasi Bazimbana akipatia huduma za afya mtoto wilayani Ntungamo nchini Uganda.
UNICEF Video/Uganda

UNICEF yawawezesha wahudumu wa afya wa vijiji Uganda kupambana na malaria

Malaria ni moja ya magonjwa hatari zaidi duniani ikielezwa na ripoiti ya mwaka 2022 ya shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO kuwa ilikatili maisha ya watu 619,000 duniani kote mwaka 2021 na waliougua ugonjwa huo kufikia milioni 247. Shirika hilo linasema asilimia kubwa ya vifo na wagonjwa wako barani Afrika hasa Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Sauti
4'9"

08 MEI 2023

Hii leo jaridani tanaangazia Jukwaa la Umoja wa Mataifa la misitu linaloendelea hapa makao makuu, vita dhidi ya ukimwi Moldova. Makala tunakupeleka nchini Uganda na Mashinani nchini Rwanda, kulikoni?

Sauti
13'32"
Mtoto akipatiwa tiba dhidi ya malaria kwenye kituo cha afya cha Gracia kwenye mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
UN News/George Musubao

Malaria na changamoto kwa wakazi wa Beni, DRC

Hii leo ikiwa ni siku ya Malaria duniani, huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, jinamizi la Malaria bado linatikisa taifa hilo ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni , WHO, Kanda ya Afrika linasema, asilimia 96 ya wagonjwa wa Malaria duniani kwa mwaka 2022 walikuwa katika nchi 29 ikiwemo DRC.