Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Msafiri Zawose aendelea kupigia chepuo muziki wa asili Tanzania

Marimba. (Picha: UNESCO)

Msafiri Zawose aendelea kupigia chepuo muziki wa asili Tanzania

Muziki wa asili umekuwa haupatiwi kipaumbele na vijana wengi maeneo mbali mbali duniani licha ya kuwa ni sehemu ya utamaduni wao kwani unazungumzia asili yao. Lakini hali ni tofauti kwa mwanamuziki wa muziki wa asili kutoka nchini Tanzania  Msafiri Zawose ambaye licha ya vijana wenzake wengi kujikita katika muziki wa kizazi kipya almaarufu  bongo fleva yeye ameamua kuitangaza nchi yake kupitia muziki asilia. Je anafanya nini? Namkeshe Msangi wa Radio washirika Voice of Afrika kutoka Korogwe Tanzania amezungumza naye katika makala hii ya midundo.