Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makumbi ya nazi huniingizia kipato na kuwasomesha watoto-Bahati

Makumbi ya nazi huniingizia kipato na kuwasomesha watoto-Bahati

Makumbi ya nazi ambayo mara nyingi hutupwa baada ya kufuliwa kwa nazi, na hivyo kusababisha uchafu wa mazingira, yanatumiwa na mjasiriamali mwanamke mkoani Tanga nchini Tanzania, kujinufaisha kwa kipato na hivyo kutunza mazingira.

Hii ni sehemu ya shuhuda za wanawake kuhusu namna wanavyokabiliana na changamoto za kazi katika dunia inayobadilika kila uchao, ikiwa ni kuelekea siku ya wanawake duniani hapo Machi nane. Maajabu Ally wa redio washirika Pangani Fm ya Tanga, amemtembela Bi Bahati Sudi na kuzungumza naye katika makala ifuatayo.