Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano wa polisi umetujenga kuimarisha usalama DRC: IGP Bisengimana

Mkutano wa polisi umetujenga kuimarisha usalama DRC: IGP Bisengimana

Mwishoni mwa juma lililopita, wakuu wa polisi kutoka kote duniani walikutana hapa New York kujadili nafasi ya polisi katika ulinzi wa amani. Bara la Afrika hususani nchi za Maziwa Makuu ziliwakilishwa vyema.

Joseph Msami wa idhaa hii amefuatilia mkutano huo na kuzungumza na mkuu wa jeshi la polisi kutoka Jamhuri ya Kidemokraia ya Kongo DRC Charles Bisengimana anayeanza kueleza umuhimu wa mkutano huo.