Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mazungumzo ya pande kinzani Syria kurejelewa Machi 9

Mazungumzo ya pande kinzani Syria kurejelewa Machi 9

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Syria, Staffan de Mistura, ametangaza leo kuwa mazungumzo ya amani baina ya pande kinzani za Syria yatarejelewa mnamo tarehe tisa Machi mwaka huu.

Awali, mazungumzo hayo yalikuwa yamepangwa kuanza tena tarehe saba Machi, lakini sasa yamehamishiwa tarehe tisa Machi ili kuruhusu muda zaidi wa kushughulikia masuala ya kivifaa na kiutendaji.

Taarifa kutoka ofisi ya mjumbe huyo imesema kwamba Bwana de Mistura anatazamia kuona washiriki wakimakinika katika mazungumzo hayo, kwa matarajio ya kutekeleza azimio namba 2254 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.