Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Okestra kutoka Venezuela yapigia chepuo amani

Okestra kutoka Venezuela yapigia chepuo amani

Katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa wiki hii kumefanyika tumbuizo la muziki kwa ajili ya kupigia chepuo amani. Amani japo ni neno lenye herufi tano, bado imesalia kuwa ndoto kwa wakazi wengi duniani wakati huu ambapo watu zaidi ya Milioni 123 wamefurushwa makwao kutokana na mizozo iwe ya kiasili au inayosababishwa na binadamu. Tamasha hilo lilihusisha okestra kutoka Venezuela na kwa yaliyojiri tuungane na Assumpta Massoi kwenye makala hii.