Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Michezo huvunja mipaka ya ubaguzi:UM

Michezo huvunja mipaka ya ubaguzi:UM

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya michezo kwa maendeleo na amani, na kamisheni ya haki za binadamu OHCHR kwa kushirikiana na nchi kadhaa zimeandaa tukio michuano ya mpira wa miguu sambamba na siku ya kimataifa ya haki za binadamu inayoadhimishwa kila tarehe 10 Disemba.

Ni tukio lililovunja mipaka ya aina zote za ubaguzi wa kila aina ambapo watu wa rangi, historia na hata mataifa mbalimbali , walijumuika. Ungana na Joseph Msami aliyeandaa makala ifuatayo.