Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Amani na usalama wa kimataifa vyajadiliwa

Amani na usalama wa kimataifa vyajadiliwa

Mjadala kuhusu amani na usalama  wa kimataifa umefanyika hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa wakati Umoja huo ukiadhimisha miaka 7o tangu kuanzishwa kwake.

Akichangia katika mjadala huo Rais wa Baraza Kuu  Mogens Lykketoft  amesema lazima chombo hicho kitatue changamoto za amani na usalama zinazotatiza dunia ikiwamo vikundi vya kigaidi na misimamo mikali, kwani bila  kufanya hivyo dhana ya maendeleo haitatimia.

Kadhalika akazungumzia changamoto ya wahamiaji inayoikumba dunia kwa sasa akisema .

(SAUTI)

‘‘Jukumu letu katika amani na usalama, haki za binadmu na maendeleo lazima lieleze namna ya kushughulikia janga la wakimbizi . Ni muhimu tupitishe njia  madhubuti katika yote tunayofanya .’’