Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ushirikiano wa kimataifa wahitajika ili kutunza bayonuai baharini: UNEP

Ushirikiano wa kimataifa wahitajika ili kutunza bayonuai baharini: UNEP

Hifadhi ya bayoanuai iliyopo baharini ni changamoto kubwa hasa wakati ambapo asilimia 64 ya maeneo ya bahari hayamilikiwi na nchi yoyote. Kwa mujibu wa Dixon Waruinge, mtalaam wa Shirika la Umoja wa Mataila la Mpango wa Mazingira, UNEP, ni muhimu mashirika ya kimataifa yaungane ili kubaini mbinu za kudhibiti maeneo haya.

Katika mahojiano na Priscilla Lecomte, Waruinge amezingatia pia hifadhi ya bayoanuai iliyopo kwenye maeneo yaliyo ndani ya mipaka ya nchi za ukanda wa Afrika ya Mashariki.