Kuimarika kwa huduma za afya kumesaidia katika juhudi za kufikia lengo la nne:Burundi
Burundi ni miongoni mwa nchi ambazo zinajivunia kupiga hatua katika juhudi za kupunguza vifo vya watoto walio na umri wa chini ya miaka mitano ikiwa ni lengo la nne katika malengo ya maendeleo ya milenia ya Umoja wa Mataifa.
Juhudi ambazo zimechangia katika kushuhudia kupungua kwa idadi ya vifo ni pamoja na utoaji chanjo ya kuzuia maambukizi hatari.
Katika makala ifuatayo Ramadhani Kibuga ripota wa Idhaa hii kutoka Burundi anatupeleka katika hospitali moja ili kutupatia taswira ya hali ilivyo ungana naye.