Hatudhibiti rasi ya Crimea: Balozi Sergeyev
Mwakilishi wa kudumu waUkrainekwenye Umoja wa Mataifa Yuriy Sergeyev amesema nchi yake haidhibiti eneo liitwalo Crimea na badala yake Urusi ndiyo inayotawala eneo hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari mjiniNew Yorkmuda mfupi baada ya kikao cha baraza la usalama la Umoja wa Mataifa lililojadili kuzorota kwa usalama Crimea nchiniUkraine. Balozi Sergeyev amesema licha ya kwamba inaonekana kimtizamo kuwa nch yake inatawala eneohilolakini hiyo ni nadharia pekee.
“ Hatudhibiti eneo hili, eneo lote linatawaliwa na Warusi kwa jeshi na au kwa msaada toka vikundi vya Urusi. Kwa hiyo alama hizi nyeupe uzionazo ni mtizamo kwamba rasi yote ya Crimea inadhibitiwa na Ukraine lakini ni Warusi . Ndiyo maana hatuwezi kuhakikisah kwamba hali ni shwari licha ya ukweli kwamba watu wanajaribu kuishi kwa usahihi.