Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ban atoa wito kwa wanaopigana kusitisha mapigano kwa ajili ya Olimpiki

Ban atoa wito kwa wanaopigana kusitisha mapigano kwa ajili ya Olimpiki

Normal

0

false

false

false

MicrosoftInternetExplorer4

st1\:*{behavior:url(#ieooui) }

/* Style Definitions */

table.MsoNormalTable

{mso-style-name:"Table Normal";

mso-tstyle-rowband-size:0;

mso-tstyle-colband-size:0;

mso-style-noshow:yes;

mso-style-parent:"";

mso-padding-alt:0in 5.4pt 0in 5.4pt;

mso-para-margin:0in;

mso-para-margin-bottom:.0001pt;

mso-pagination:widow-orphan;

font-size:10.0pt;

font-family:"Times New Roman";

mso-ansi-language:#0400;

mso-fareast-language:#0400;

mso-bidi-language:#0400;}

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, ametoa wito kwa pande zote zilizopo kwenye migogoro ya silaha kuweka silaha chini na kusitisha mapigano kwa ajili ya mbiu ya amani ya Olimpiki, kabla kuanza michezo ya Olimpiki ya msimu wa baridi mjini Sochi, Urusi.

Bwana Ban amesema washiriki katika michezo hiyo watabeba bendera za nchi tofauti, lakini wanakuja pamoja chini ya bendera moja ya usawa, kucheza kwa haki, kuheshimiana na kutobaguana. Ametoa wito kwa wote wanahusika katika michezo hiyo, zikiwemo serikali, makundi, mashirika na watu binafsi, kutunza na kulinda maadili hayo muhimu ya Olimpiki.

Ban amesema anapotoa mbiu ya amani mwaka huu, anawawazia watu wa Syria, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Sudan Kusini na wote wanaoteseka kutokana na machafuko yasiyo na maana, zikiwemo familia zilizowapoteza wapendwa wao katika shambulizi la bomu hivi karibuni, huko Volgograd, ambayo si mbali sana na Sochi.