WHO kutoa ripoti ya saratani kwa nchi 40 Jumatatu
Shirika la afya duniani WHO limesema litatoa ripoti ya kimataifa ya mwenendo wa saratani itakayogusia nchi 40.
Ripoti hiyo itakayotolewa Februari 3 inatarajiwa kusisitiza kwamba matibabu pekee hayawezi kushinda vita dhidi ya saratani.
Hivyo kunapaswa kuwa na juhudi zaidi za hatua za kuzuia na kudhibiti saratani. Ripoti hiyo itazinduliwa mjini London.